ILI UELEWE LAZIMA UKUBARI KUJIFUNZA, NA ILI UJIFUNZE LAZIMA KWANZA UONDOWE MISAMO AMA ITAKAIDI FULANI FULANI EIDHA YA KIDINI AMA YA KIELIMU HAPO UTAKUWA MWANAFUNZI MZURI UTAKAYE JUWA MENGI "BY SHIBITA.COM" :
SWALI LA KUJIULZA, BABELI NI NINI?, NI KITU GANI NA KILIANZA LINI NA KWANINI BABELI IMETAJWA SANA AGANO LA KALE NA AGANO JIPYA KUNA NINI HAPA? HAPANA RAFIKI KARIBU TUJIFUNZE HABARI ZA BABELI MAANA KUNA SIKU BABELI ITAANGUKA WALA HAITA SIMAMA TENAUFUNUO18:21.
Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema: “Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli utakavyotupwa chini kwa nguvu wala hautaonekana tena.
MWANZO WA BABELI.
Jina Babeli lina maana kuu mbili,maana ya kwanza ni MACHAFUKO Mwanzo 11:1-9 na maana ya pili ni LANGO LA MIUNGU AU MASHETANI kwanini ni lango la miungu kwa sababu chanzo cha ibaada ya kumwabudu shetani kilianzia pale mfano ilikuwa na mahekalu 300, madhabahu 905 ilikuwa na miumgu zaidi ya 500,chanzo soma habari za herodotus juu ya babeli anasema babeli kilikuwa ni kituo kikuu cha dini kisicho na upinzani dunia.
WAANZILISHI WA BABELI YA KALE {NIMROD MWAKA 1751 bc }
Biblia kitabu cha mwanzo kinasema mwanzo 10:8-10
Kushi akamzaa Nimrodi, akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.
9 Alikuwa hodari kuwinda wanyama mbele za Bwana. Kwa hiyo watu hunena, Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za Bwana.
10 Mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari.
11 Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala;
12 na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.
LENGO LA KUUJENGA MNARA WA BABELI.
Walitaka wakae sehemu moja kinyume na matakwa ya MUNGU.Ikumbukwe MUNGU alimuagiza Nuhu waende wakatawanyike mbele ya uso wa nchi,lakini wao wakaamua kufanya kinyume na amri ya MUNGU ili wajitwalie utukufu wao wenyewe (KIBURI).
Dhambi kubwa iliyofanya MUNGU awachafulie usemi wao ilikuwa "Na tujifanyie jina wenyewe",Je wakati huo kulikuwa nchi ambayo walikuwa wanataka kushindana nayo?je walitaka nani awasifu?kulikuwa na nchi ya jirani? ila walikuwa wanashindana na MUNGU mwenyewe.
NIMROD ALIKUWA NA MAKUNDI MATATU.
1.Kundi la kwanza lilikuwa kwa ajiri ya kumuua MUNGU
2.kundi la pili walikuwa na kazi ya kutengeneza mishalie kwa ajiri ya kumuua MUNGU
3.Kundi la mwisho kwa ajiri ya ujenzi wa babeli
Tembelea (skiba 2012) kwa mapitia .
Hapo ndipo utakapogundua kuwa Nimrodi alitaka kwenda kukaa kwenye kiti cha enzi cha MUNGU.
Hayo yote ndiyo yaliyomchukiza MUNGU na kuamua kuwachafulia usemi wao ili wapate kujifunza na kuwalazimisha kugawanyika mbele ya uso wa MUNGU.
HII INAENDA SAMBAMBA KABISA NA ANGUKO LA SHETANI KWA KUTAKA KUWA KWENYE KITI CHA ENZI CHA MUNGU
Chini ya nimrodi mambo mengi ya kishetani yaani ibaada za kishetani nyingi zilianzishwa mfano ibaada ya kuabudu jua, mwezi, sayari, wafu na masanamu mbalimbali, vile vile sherehe mbalimbali zilianzishwa kama vili ISHTAR ambyo imetoholewa na kuitwa EASTER, CHRISMASS PIA IMETOKEA HUKO NA SHEREHE NYINGINE NYINGI.