MJUE SANA MUNGU,ILI UWE NA AMANI, NDIVYO MEMA YATAKAVYOKUIJIA

IJUE ALAMA YA MNYAMA 666, NA KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI. sehemu ya kwanza.

               KITABU CHA UFUNUO 13   MAANDIKO YANASEMA KWAMBA                                                                                                                                                 1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.

2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.

4 Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye?

5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.

6 Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni.

7 Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa.

8 Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia
9 "Mtu akiwa na sikio na asikie"


   Kuwa mkristo maisha yako yote  nakisha ukapokea alama ya mnyma katika saa ya mwisho ya historia ya ulimwengu, huo utakuwa msiba mkubwa,na wakutisha sana .
Alama ya mnyama itakuwa ni hatua ya mwisho katika uasi zidi ya MUNGU, lakini  utakuwa ni uasi uliofichwa kwa werevu sana kuliko mwingine ambao shetani amewahi kuwashirikisha wanadamu katika uasi wake, litakuwa ni  jaribu lake kubwa kuliko yote ambayo amewahi kuwahusisha wanadamu kwanini?.


kwasababu ya mambo makuu matano anayoyaandaa ambayo ni 

          1.alama  ya mnyama itakuja  imeavaa ukristo.
                     2.itabuniwa wakati wa mdololo mkubwa wa uchumi
                                   3. itatangazwa wakati wa janga kubwa la badiliko la hali ya hewa
                                  4.alama ya mnyama itakuja kama suluhisho la ugaidi duniani
                               5.alama ya mnyama itakuja kama suluhisho la magonjwa dunia
Wakati huo itaonekana  kuwa ni laziama  watu wote waungane ili kuepusha janga la ulimwengu mziama na itaonekana kwamba alama ya mnyama  ndio ufumbuzi pekee, hivyo neno la MUNGU hutuambia kuwa  mtu  yeyote atakayepinga  atatishwa vikali na mamlaka hiyo tunayasoma yote haya katika kitabu cha ufunuo 13 na 14

             LAKINI MASWALI YA KUJIULIZA NI HAYA,

               1.ALAMA YA MNYAMA NI KITU GANI HASA.

2 NA KINAKUWAKUWAJE HASA, JE?

3.  NI NAMBA HALISI  YAANI 666.

                               4.AMA NI KITU FULANI KILICHOFICHIKA KATIKA MAANA HALISI YA UNABII.

hakika mada hii itaendelea hadi mwisho wa maswali yetu tajwa hapo juu 
MUNGU AKUBARIKI, ZAIDI AKUEPUSHE NA HII HOJA YA MPINGA KRISTO YAANI ALAMA YA MNYAMA  napatikana kwa namba za simu kama utakuwa na maswali  piga simu namba   0763371047
                                                            





                                                                                             

Subscribe to receive free email updates: